Ezekiel 37:15-20

15Neno la Bwana likanijia kusema: 16 a“Mwanadamu, chukua fimbo na uandike juu yake, ‘Hii ni kwa ajili ya Yuda na Waisraeli waliofungamana naye.’ Kisha chukua fimbo nyingine, uandike juu yake, ‘Fimbo ya Efraimu, ni kwa ajili ya Yusufu na nyumba yote ya Israeli wanaofungamana naye.’ 17 bZiunganishe pamoja kuwa fimbo moja ili kwamba ziwe fimbo moja katika mkono wako.

18 c“Watu wako watakapokuuliza, ‘Je, hutatuambia ni nini maana ya jambo hili?’ 19 dWaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaichukua fimbo ya Yusufu, iliyoko mikononi mwa Efraimu na ya makabila ya Israeli yanayofungamana naye na kuiunganisha na fimbo ya Yuda, nikizifanya kuwa fimbo moja, nao watakuwa wamoja katika mkono wangu.’ 20 eInua mbele ya macho yao zile fimbo ulizoziandika
Copyright information for SwhKC